Mafunzo

Kutokana na kuanza kukua kwa teknolojia ya habari na mawasiliano hapa Tanzania na Mafunzo mbalimbali yanayotolewa katika taaluma ya Kompyuta bado hakuna mafunzo rasmi yanayoelekeza kupatikana kwa wataalam katika sanaa ya kompyuta pia utayarishaji filamu na vipindi mbalimbali vya televisheni hapa nchini. Kampuni yetu imedhamiria kuwekeza katika taasisi ya mafunzo yenye kiwango cha kimataifa ili kutoa mchango katika sekta ya utayarishaji filamu ambayo kwa siku za hivi karibuni imeanza kupata mwelekeo mpya hivyo kuwepo kwetu kutaleta thamani zaidi na kuingiza kazi zilizotayarishwa Tanzania katika soko la kimataifa na hivyo kuipatia nchi fedha za kigeni na kuitangaza katika anga za kimataifa. Kwa jinsi hii kizazi cha wasanii, watayarishaji filamu na wadau wengine watapata matumaini mapya ya siku za usoni. Taasisi yetu ya mafunzo itazingatia uwezo wa mwanafunzi kitaaluma na hivyo kuwapokea hata wale wenye uwezo mdogo wa fedha lakini wenye vipaji na uwezo wa kufuata mafunzo. Tuna amini ya kwamba vijana wa Tanzania ni hodari na wanaopenda kujifunza wakipewa fursa na dira sahihi.