Kampuni
Keystone
Animation Ltd. ni kampuni iliyoanzishwa na mwana historia
na mtayarishaji filamu wa Kijerumani aitwaye Christoph Neubauer
akishirikiana na mtanzania jijini
Dar-es-salaam – Jamhuri ya Muungano wa Tanzania . Muasisi
huyu anatumaini kwamba kuanzishwa na kufanya kazi kwa mafanikio
kwa kampuni hii kutavutia wawekezaji wengi zaidi kutoka
nje kuja kuwekeza katika nyanja ya teknolojia ya sanaa ya
kompyuta (computer graphics and animations) pia fani ya
utayarishaji na utengenezaji filamu.
Mtazamo
Mtazamo wetu umejikita
katika utayarishaji wa filamu za mafunzo (documentaries)
Kutokana na mada mbalimbali za kihistoria zilizo fanyiwa
utafiti wa kina kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya sanaa
ya 3D computer animations. Ujenzi mpya wa sanifu za kihistoria
zilizotoweka kutokana na ukale wake ndio mhimili mkuu wa
kazi yetu. Yote haya yanafanyika huku tukizingatia umuhimu
na usahihi wa historia.
Ubora
na Viwango
Ili kuhakikisha
ubora na viwango vinafikiwa katika filamu tunazotayarisha,
kampuni hutumia huduma za utengenezaji au uchapishaji kutoka
kampuni mwenza ijulikanayo kama "Christoph Neubauer
publishing" iliyoko Ujerumani, na ni kwa jinsi hii
tu tunaweza kufikia ufanisi wa juu katika ubora na viwango
vitakiwavyo kimataifa.
Changamoto
nchini Tanzania
Kwa vile
lengo letu kubwa ni kujikita katika utayarishaji na utengenezaji
wa filamu za kimafunzo na hasa zile zenye mwelekeo wa kihistoria
na kuziweka katika mfumo wa DVD tayari kwa mauzo, katika
soko la kimataifa, zipo changamoto kadhaa zinazo jitokeza
hapa nchini Tanzania. Tanzania
, ikiwa nchi mojawapo katika mataifa yanayoendelea ya ulimwengu
wa tatu Utafiti
unaonyesha kwamba, ni asilimia kumi tu (10%) ya watu wote
wenye kufikiwa na huduma ya umeme, ambapo sehemu kubwa wapo
mijini na ni asilimia mbili tu (2%) ya watu wenye kupata
huduma ya teknolojia ya habari kupitia mtandao wa kompyuta
(Internet) Hali
hii inaleta changamoto kubwa hasa kwa kampuni ambayo shughuli
zake zinategemea zaidi umeme wa uhakika, teknolojia ya kompyuta,
habari na mawasiliano Yenye
kuwepo wakati wote.Changamoto nyingine inatokana na upungufu
au ukosefu wa wataalam waliofuzu vizuri Katika
nyanja za taaluma ya sanaa ya kompyuta (computer graphics
and animation) na utayarishaji na utengenezaji wa filamu.
Ili
kukabiliana na changamoto hii, kampuni inadhamiria kuwekeza
katika kutoa mafunzo mbalimbali ya kitaaluma ili kujenga
uwezo wa rasilimali watu nchini Tanzania. Kama
ilivyo kwa nchi nyingi zinazoendelea, Tanzania nayo haijajiunga
na taratibu za Kimataifa zinazo ratibu nambari maalumu za
bidhaa katika biashara. (Global Trade Item Number) ambazo
huwezesha uingizaji wa bidhaa katika soko la kimataifa.
Kutokana
na changamoto hii mauzo ya filamu zitokazo nchini kwenda
kwenye soko pana duniani, hayatawezekana kwa kuwa vigezo
hivyo muhimu vinapaswa kuzingatiwa kwanza.Kwa
sababu hii kampuni ya Keystone Animation Ltd kupitia kampuni
dada iliyoko Ujerumani ita chapisha na kuratibu kazi zote
na kuziingiza katika soko la kimataifa Kwa
urahisi na faida.