Filamu
hapa nchini
Kama
zilivyo nchi nyingi katika bara la Afrika ambapo utayarishaji
na utengenezaji wa filamu za ndani haujapata mwamko mkubwa,
hapa Tanzania hali si tofauti tumeshuhudia filamu nyingi
zinazohusu habari za ndani ya nchi zikitengenezwa na watu
wa nje, ambapo mara nyingine zimeibua mijadala na misuguano
kutokana na kukinzana na masuala muhimu ya ukweli ,maadili
na uhalisi wa mada. Tungependa
kushiriki katika uibuaji, utayarishaji na utengenezaji wa
filamu za Kitanzania kwa kushirikiana na wadau mbalimbali
na hasa wanahabari , waongozaji, na watayarishaji wa filamu
ambapo tutapokea tahariri zao kisha kuchambua mada itakayokua
na maudhui, ujumbe au mawazo yanayokubalika na kisha kushiriki
katika uzalishaji wake kwa viwango na ubora wa kimataifa
ili kukuza na kutangaza jina la Tanzania na mtengenezaji
wa filamu husika,tutaipeleka kwenye vituo vya televisheni
mbalimbali duniani ili ipate kuonyeshwa na kuwa tumesaidia
kuitangaza. Pia filamu hiyo itawekwa kwenye tovuti yetu
ambapo itatangazwa duniani wakati wote.
Keystone
Animation Ltd inajivunia mafanikio iliyofikia baada ya kuwa
imetayarisha na kuingiza sokoni filamu zake zinazohusu historia
ya mji wa Berlin huko Ujerumani ambazo zimepokelewa vema
na kupata mauzo ulaya na Marekani. Ni kwa uzoefu huu tungependa
kuandaa filamu au vipindi mbalimbali vya televisheni kuuelezea
ulimwengu juu ya mafanikio ya Afrika na changamoto zilizopo
kufikia malengo ya millennia.